Posts

Showing posts from November, 2023

AJALI YA NDEGE MBILI, WATU 60 WANUSURIKA

Image
    Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limethibitisha kutokea kwa ajali mbili za Ndege ( muda tofauti) leo katika uwanja wa Ndege wa Kikoboga uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Mikumi ambapo zaidi ya Watu 60 kwenye Ndege zote mbili wamenusurika. TANAPA imesema Ndege ya kwanza ya Unity Air 5H-MJH aina ya Embraer 120 majira ya saa 3:40 asubuhi ikiwa na Abiria 30, Marubani wawili na Mhudumu mmoja ikitokea Zanzibar ilipata tatizo la kiufundi wakati wa kutua kiwanjani hapo lakini kwa juhudi kubwa za Marubani na Maafisa wa kiwanja hicho hakuna madhara yaliyojitokeza ambapo Abira wote, Marubani na Muhudumu mmoja wako salama na wanaendelea na ratiba yao ya Utalii hifadhini.               Moja ya ndege zilizopata ajali       Katika taarifa ya pili, TANAPA imethibitisha kutokea kwa ajali ya pili leoleo saa 9:30 alasiri ikihusisha Ndege ya Kampuni ya Unity Air 5H-FLM aina ya E120 ikiwa na Abiria 30, Mar...

DUGANGE AMEWATAKA VIONGOZI WA SEKTA YA AFYA WAWAELEZE WANANCHI MAFANIKIO YA SEKTA HII NCHINI ILI KUONA SERIKALI INAVYOBORESHA.

Image
DODOMA;      Viongozi wa sekta ya afya wametakiwa kuwaeleza wananchi mafanikio yanayopatikana katika sekta ya afya  ili kufahamu namna serikali ilivyoboresha huduma za afya nchini. Naibu waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Festo Dugange  ametoa maagizo hayo leo alipokuwa akifungua kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mpango wa Afua za Takwimu za Bidhaa za Afya (IMPACT) jijini Dodoma . Dkt.Dugange amesema kuwa serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe.Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya kwa kujenga vituo vya kutolea huduma za afya,ununuzi wa dawa na vifaa tiba pamoja na kuajiri wahudumu wa afya hivyo ni jukumu la kila kiongozi kuyasemea mafanikio hayo kwa wananchi. Akizungumzia kuhusu vifaa tiba vilivyonunuliwa na serikali,Dkt.Dugange amewaagiza wahudumu wote kuvitunza vifaa  hivyo ili viweze kudumu kwa muda mrefu...

SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI, DKT. GWAJIMA ASIMAMA NA MASHUJAA.

Image
"Wekeza Kuzuia Ukatili wa Kijinsia". Mgeni rasmi alikuwa  Dkt. Gwajima D  , Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Siku 16 za Kupinga Ukatili Wa Kijinsia ni Kampeni ya Kimataifa inayoadhimishwa kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 10 (Siku ya Haki za Binadamu) kila Mwaka ili kuongeza wito wa kutokomeza aina zote za Ukatili wa Kijinsia Ukatili mwingi dhidi ya Wanawake/Wasichana unafanywa na Watu wa karibu ikiwemo Wenza wao au Wenza walioachana nao. Kauli mbiu Wekeza: Kuzuia Ukatili wa Kijinsia ,  Kauli mbiu hii ni wito kwa kila mmoja wetu kutumia nafasi aliyonayo katika familia, jamii ama taasisi kuchukua hatua thabiti kuzuia vitendo vya ukatili wa kijinsia. Kaulimbiu hii pia inasisitiza jamii, taasisi za umma na za binafsi kuwa na hatua za makusudi za kuongeza ulinzi kwa wanawake na watoto dhidi ya ukatili wa kijinsia. Wito huu pia unasisitiza ya kwamba vitendo vya ukatili vinazuilika na kinga ni bora kuliko tiba. CHIMBUKO Chimbu...

KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA MBINGA YAKABIDHI VIFAA TIBA KWA WANANCHI WA KATA YA MATIRI VILIVYOTOLEWA NA MHE JUDITH KAPINGA (MB)NAIBU WAZIRI WA NISHATI

Image
    Mbinga; Tarehe 26.11.2023 Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbinga ikiongozwa na  Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Mbinga Comrade BASHIRU MADODI imefika katika Kituo cha Afya MATIRI na kuongea na Wananchi wa Kata ya Matiri waliohudhuria katika hafla hiyo ya Makabidhiano ya Vifaa hivyo Tiba katika Kituo Cha Afya Matiri.      Awali katika Mkutano huo wa Wananchi Mhe Diwani wa Kata ya Matiri  WILLIAM MSAFIRI MBWAMBO aliwakaribisha Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Mbinga wakiongozwa na Katibu wa Chama  Comrade Bashiru Madodi.       Mhe Diwani Mbwambo wa Kata hiyo ya Matiri alimpongeza sana Mhe.Judith Kapinga (Mb) Naibu Waziri kwa moyo wake wa upendo aliouonyesha kwa Wanambinga hususani katika kusaidia Kutoa Vifaa Tiba kwa Wananchi,kwani jambo hilo ni la kipekee sana na    na linahitaji moyo.  Mhe Diwani Mbwambo alimshukuru sana Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu Hassan kwa ...

SHOO KUBWA YA MAONESHO YA VICHEKESHO VYA WIMA (STAND UP COMEDY) KUWAHI KUTOKEA, DAS WILAYA YA MBEA AKEMEA MASHOGA.

Image
    Ikiwa ni msimu wa pili wa Mbeya Comedy Festival, ni Tar 24November. 2023 ambapo Show hiyo kubwa iliyokuwa imesubiriwa na wakazi wa Mbeya na nje ya mipaka yake kwa takribani miezi mitatu. Hatimaye imeweza kufikia kilele hapo jana Tar 24Nov, Ijumaa hii ndani ya Ukumbi wa Tughimbe Hall.  Huwezi kutokuiweka kwenye miongoni mwa Show kubwa kuwahi kufanyika nyanda za juu kusini, hasa Mkoa wa Mbeya na wilaya zake.     Mgeni rasmi alikuwa Mh. Dkt Tulia Ackson ambaye ni Mkurugenzi wa Tulia Trust, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Spika wa Bubge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa IPU. Japo kutokana na majukumu aliweza kumtuma Muwakilishi DED wa Wilaya ya Mbeya, ambaye wakati wa kutoa salamu aliweza kuwaasa vijana juu ya nafasi ya kujiwekeza. " Kwa miaka 10 iliyopita huko nyuma, kumpata shoga ilikuwa ni vigumu saana. Lakini sasa hivi vijana kwakuwa hawataki kufanya kazi za mapambano, wala kujituma ili...

JE, UNATAMBUA KUWA MADHARA YA UPWEKE NI SAWA NA KUVUTA SIGARA 15 KWA SIKU?

Image
   Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa hali ya upweke imekuwa kipaumbele cha afya duniani ambapo limezindua Tume mpya ya ā€˜Uhusiano wa Kijamii’ kwa ajili ya kushughulikia suala hilo huku ikielezwa kuwa athari za upweke zinaweza kuwa mbaya kama kuvuta sigara 15 kwa siku na ni kubwa kuliko athari zinazohusiana na unene na kutofanya mazoezi ya mwili. CNN imeripoti kuwa Tume hiyo inalenga kushughulikia upweke kama tishio kubwa la kiafya, kukuza na kuwezesha mahusiano ya kijamii kuwa yenye kipaumbele na kuharakisha utafutaji wa suluhisho la upweke duniani. Tume hiyo inaongozwa na Daktari Mkuu wa Upasuaji wa Marekani Dkt. Vivek Murthy na Mjumbe wa Vijana wa Umoja wa Afrika Chido Mpemba huku ikijumuisha Mawakili 11 na Mawaziri wa Serikali kama vile Ralph Regenvanu, Waziri wa kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa nchini Vanuatu, na Ayuko Kato, kutokea nchini Japan. Ndani ya miaka mitatu Tume itatoa ripoti itakayobainisha jinsi upweke n...

AFYA YA AKILI NI MSINGI MKUU WA KUPAMBANA NA MATUKIO YOTE YA UKATILI, NI NJIA PEKEE YA KULETA USAWA NA MAENDELEO BORA KWENYE JAMII:

Image
      Ripoti ilitolewa leo huko Geneva, Uswisi na shirika la  Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO ikiwa ni tathmini kubwa zaidi kutolewa tangu kuanza kwa karne hii ya 21. Kilichomo kwenye ripoti hiyo ni mwongozo kwa serikali, wasomi, wataalamu wa afya, mashirika ya kiraia na wengineo katika kusaidia harakati za kuleta marekebisho makubwa katika afya ya akili ambayo sasa ni tatizo kubwa. Ukubwa wa tatizo Mwaka 2019, takriban iwatu bilioni 1 wakiwemo asilimia 14 ya vijana wote barurbaru duniani walikuwa wanaishi na tatizo la akili. Tatizo hilo la akili lilisababisha mtu 1 kati ya 100 kujiua na asilimia 58 ya watu kujiua ni kwa watu wenye umri wa chini ya miaka 50. WHO inasema tatizo la akili ni sababu inayoongoza ya ulemavu na watu tatizo kubwa la afya ya akili kwa wastani hufariki dunia miaka 10  hadi 20 mapema zaidi kuliko watu wa kawaida kutokana na magonjwa ya mwili yanayoweza kuzuilika.      Vichocheo vya  magonjwa ya ak...

BODI YA MTETEZI WA MAMA MBEYA YAFIKA WILAYA YA MBARALI KUIMARISHA UONGOZI TAASISI MASHINA, TAWI KATA.

Image
Mbarali, Mbeya Bodi ya Mtetezi wa Mama Mkoa wa Mbeya imeendelea na zoezi lake la kuimarisha safu za Uongozi kwa Kila mitaa na kata Kwa Mkoa mzima wa Mbeya. Na zoezi hilo lenye lengo la kutafuta Wananchi wazalendo bila kujali itikadi zao za vyama vya Siasa Dini, ukanda ama ukabila agenda ni kumuongezea Kura za kutosha Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.  Nae Mwenyekiti wa Bodi Mkoa Ndg. Ibrahim Shermuhamed Mwakabwanga amelezea dira na dhamira ya Mtetezi wa Mama Kwa Mkoa wa Mbeya. Kwa Kila Mtetezi wa Mama ni lazima awe na shughuli za kufanya Ili aweze kujikwamua kiuchumi hasa akiwa katika majukumu yake ya kumtangaza Mhe. Rasi juu ya maendeleo yanayo patikana kupitia serikali yake ya awamu ya sita, kwani Kila mtaa na Kijiji Kuna Maafisa wa serikali wanao toa huduma mbalimbali, Kila Kijiji na kata Kuna vituo vya afya na zahanati, sasa Kila wilaya Mama Samia kajenga Vyuo vya Veta ikiwepo na Wilaya ya Mbarali. Katika picha ni Viongozi ng...

WANAWAKE WA AFRIKA WAMPA TUZO YA HESHIMA BALOZI GETRUDE MONGELLA, ISHARA YA KUTAMBUA MCHANGO WAKE KWENYE UONGOZI AKIWA KAMA MWANAMKE.

Image
Dar Es Salaam Wito umetolewa kwa Wanawake kujiamini na kujipambanua kitaifa na kimataifa kwenye kusimamia ajenda za maendeleo yenye usawa wa kijinsia na kupinga ukatili wa kijinsia na kwa watoto. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ametoa wito huo wakati wa hafla ya kumkabidhi Mhe. Balozi Dkt. Getrude Mongella Tuzo ya Heshima, iliyofanyika jijini Dar Es Salaam Novemba 18, 2023. Tuzo hiyo iliyotolewa na Umoja wa Wanawake wa nchi Huru za Afrika (PAWO-Africa) Julai 31, 2022 nchini Namibia, lengo lake ni kutambua mchango wa Balozi Getrude kwenye uongozi wa ngazi mbalimbali za Kimataifa ikiwemo kuwa rais wa utetezi wa wanawake Afrika na rais wa kwanza wa Bunge la Afrika. Vilevile, Balozi Getrude amekuwa Mshauri Mwandamizi na Katibu Mtendaji wa Kamisheni Uchumi ya Afrika katika masuala ya Jinsia, Mlezi wa Asasi za Kiraia zisizo za Kiserikali pamoja na kusimamia Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya...

BODI YA MTETEZI WA MAMA MKOA WA MBEYA WAFANYA ZIARA CHUNYA, WAFANYA KIKAO NA MKUU WA WILAYA NA KUFIKA OFISI ZA MKURUGENZI WA WILAYANI HUMO

Image
       Mwenyekiti wa Bodi Mtetezi wa Mama Mkoa wa Mbeya Ndg. Ibrahim Shermuhamed Mwakabwanga  akiwa na katibu wake Bodi hiyo Ndg. Asajile Mwankina  wamefanikiwa kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Simon Mayeka  na kufanya utambulisho pamoja na Kikao kifupi       Aidha katika kikao hicho mambo kadha wakadha yamejadiliwa ikiwemo na somo la uzalendo pamoja na kulinda heshima ya Mkuu wa Nchi ambae ndiye Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan , upande wa Bodi wameeleza dira na mpango kazi wao wa kuhakikisha Mama anapata kura za kutosha ifikapo mwaka 2025. Na katika kufanya kazi za Taasisi ni kwamba Watetezi watafanya kazi zao kijamii, kiuchumi pamoja na Siasa inayo mlenga Mama wa Taifa. Mkuu wa wilaya amewapongeza sana Viongozi hao walio wakilisha Viongozi wengine kutoka Taasisi hiyo.     Pichani ni Katibu wa Mkoa Mtetezi wa Mama Daudi Yilanga, Katibu uhamasishaji Mkoa Sharifa Mwal...

SMAUJATA YAFANYA UPATANISHO WA NDOA KWA WAPENDANAO JIJINI MBEYA, VITA YA UKATILI NI MAISHA.

Image
     Uongozi wa SMAUJATA Mkoa wa Mbeya umefika  kata ya Iganjo mtaa wa ikhanga Halmashauri ya Jiji la Mbeya Lengo kuu la ujio wa Viongozi hao ni mra baada ya kupokea taarifa kutoka kwa msamaria mwema ambae jina lake tuna lihifadhi  Kwa Taarifa zilizo ripotiwa ni kuwa mwanaume mmoja ambae jina lake linahifadhiwa alikimbia familia na kutekeleza mama na watoto kwa Muda wa miaka mitatu, ndipo SMAUJATA ilipo amua kuvunja ukimya na kumtafuta Baba wa familia na kumpa elimu dhidi ya ukatili na ndipo alipo gundua kuwa anafanya makosa.  Mwanaume huyo baada ya Elimu kaomba Msamaha na kuto rudia Tena kukimbia familia.  Mashujaa hao katika ziara hiyo ya kutokomeza ukatili katika jamii wameongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa na Usajili Mkoa  Asia Boniphace, Loveness Chatanda, Christophe Palange Viongozi wa wilaya Alie pokea ugeni huo ni Mwenyekiti wa Ufuatiliaji na Utekelezaji  viongozi Maiko Makunja pamoja na Shujaa ngazi ya Kata.  ...

MBEYA COMEDY FESTIVAL NA DREAM FM MSIMU WA PILI 2023, NI MAGEUZI YA SANAA NYANDA ZA JUU KUSINI

Image
     Zikuwa zimebakia siku chache kuelekea kwenye kilele cha MBEYA STANDUP COMEDY FESTIVAL 2023, leo viongozi wa Festival hiyo wamefika kwenye kituo cha radio Dream FM kilicho katikati ya Jiji la Mbeya na kuongelea ukubwa wa tukio hilo.       "Mkoa wa Mbeya mbali na kubarikiwa Upatikanaji wa Vyakula, Pesa na Viongozi wakubwa Kitaifa na kimataifa ambao kila wanapopita huacha mbegu na alama njema, Mbeya pia imebarikiwa kuwa na vipaji vikubwa vya Sanaa. Mbeya ina watu wenye vipaji vya kushangaza, sasa sisi tunataka hiyo siku kwakuwa ni Festival basi watu waje waone kila aina ya Sanaa japo kubwa zaidi watu watacheka saana hiyo siku." Innopresenter wa Mbeya StandUp Comedy Festival.    Tickets zipo kila mahali yaani ulipo basi nazo zipo, usipange kukosa hii sio ya kusimuliwa.        Mbeya StandUp Comedy Festival 2023 itafanyika kwenye ukumbi wa TUGHIMBE HALL, uliopo Mafyati Jijini Mbeya...

TAIFA STARS NDANI YA MOROCCO KUZOA USHINDI ILI KUPATA TIKETI YA KUSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2026

Image
          TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeondoka hapo jana kwenda Morocco kwa ajili ya mchezo wake wa kwanza wa Kundi E kufuzu Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2026 zinazoandaliwa kwa pamoja na nchi za Canada, Mexico na Marekani.            Taifa Stars watakuwa wageni wa Niger Jumamosi Uwanja Marrakech nchini Morocco, kabla ya kuwakaribisha Morocco katika mchezo wa pili wa Kundi hilo Novemba 21, mwaka huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.      Pamoja na Taifa Stars, Niger na Morocco timu nyingine zilizopo Kundi E ni Kongo  na Zambia, wakati Eritrea imejitoa. Timu tisa zitakazoongoza makundi zitafuzu moja kwa moja kuiwakilisha kwenye Fainali za Kombe la Dunia, wakati washindi wa pili bora wanne wa makundi watamenyana katika Nusu Fainali na Fainali na mshindi atakwenda kushiriki mchujo wa Mabara kuwania nafasi ya kwenda Kombe la Dunia pia.         ...