SHUJAA BULUGU ATOA SHUKRANI KWA KAMANDA WA POLISI (RPC) MKOA WA MWANZA KWA MWALIKO WAKE KWA SMAUJATA KUSHIRIKI SHEREHE YA UVISHWAJI NISHANI KWA MAAFISA , WAKAGUZI , NA ASKARI WA KANDA YA ZIWA
Mwenyekiti SMAUJATA Taifa Shujaa Sospeter Mosewe Bulugu analipongeza na kulishukuru jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza kwa Mwaliko huo ambapo Mwenyekiti SMAUJATA Mkoa wa Mwanza Shujaa Gasto Alex Didas (Aliyevaa Suti nyeusi Mstari wa Pili) kwa niaba ya Mwenyekiti SMAUJATA Taifa amehudhuria na Kushiriki.
Katika Sherehe hiyo, Mgeni Rasmi ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Afande IGP Camillius Mongoso Wambura ambapo amewavisha nishani Maafisa na Maaskari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kwa Niaba ya Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan .
Jumuiya ya SMAUJATA Itaendelea Kufanya Kazi na Kushirikiana Bega kwa Bega (Sako kwa Bako) na Jeshi la Polisi Nchini katika Mapambano dhidi ya Vitendo vya ukatili na Katika Shughuli zote za Ustawi wa Jamii.
Shujaa Sospeter Mosewe Bulugu,
Mwenyekiti SMAUJATA Taifa
By
Wamzi Media
Comments
Post a Comment