Posts

TAASISI YA TULIA TRUST YATOA MIFUKO 50 YA SARUJI SHULE YA MSINGI IKULE MASEBE RUNGWE

Image
  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust imetoa msaada wa mifuko hamsini ya saruji kwa shule ya Msingi Ikule Kata ya Masebe Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya kwa ajili ya kukarabati ofisi ya walimu ambapo kwa sasa wanatumia moja ya darasa kama ofisi. Msaada huo umekabidhiwa na Afisa Habari wa Taasisi ya Tulia Trust Joshua Mwakanolo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Tulia Trust Dkt Tulia Ackson. Mwakanolo amesema Taasisi ilipokea maombi kutoka uongozi wa shule hiyo hivyo kwa kutambua umuhimu wa elimu Taasisi imewiwa kutoa msaada huo Ili kuchochea ubora wa elimu sanjari na kuungana na Serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu. Innocent Atilyo ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo amesema sehemu kubwa ya shule hiyo imejengwa kwa nguvu za wananchi ikiwa na madarasa saba na jumla ya watoto zaidi ya mia mbili thelathini ambapo Serikali imetoa milioni thelathini na tano n...

RAIS WA IPU MH. DKT. TULIA NA RAIS WA HUNGARY WAJADILI HALI YA AMANI DUNIANI

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 8 Oktoba, 2024 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Hungary, Mhe. Tamas Sulyok katika Ikulu ya nchi hiyo iliyopo Jijini Budapest. Katika mazungumzo yao, Viongozi hao walijadili njia bora za kuimarisha ushirikiano kati ya mataifa haya mawili, Tanzania na Hungary, katika sekta mbalimbali hususani kilimo, utalii, biashara na maji. Rais Sulyok alitumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Dkt. Tulia kwa juhudi zake za dhati katika kuendeleza amani duniani, hususani katika maeneo yanayokumbwa na migogoro mikubwa. Aidha, walizungumzia pia masuala yanayohusu misingi na malengo ya IPU, ambapo Mhe. Sulyok aliahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na kuwa mstari wa mbele katika kuendeleza ajenda zote za IPU. Ifahamike kuwa kati ya nchi nane zilizounga mkono kuanzishwa kwa IPU katika mkutano uliofanyika tarehe 29 na 30 Juni 1889 nchini Ufaransa, Hungary ilikuwa miongoni mwa...

DKT. TULIA ALIVYO WEZESHA MASOMO KWA VIJANA WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU MBEYA, SONGWE NA RUVUMA.

Image
Vijana watano kutoka mikoa ya Mbeya, Songwe na Ruvuma waliokua masomoni Nchini Nigeria Kwa ufahili wa Spika wa bunge la Tanzania na mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini Dkt Tulia Ackson kupitia taasisi yake ya Tulia Trust, wamerejea Kwa mara ya Kwanza baada ya miaka sita tangu walipoondoka mwaka 2018 walipokwenda kujiunga na kidato Cha kwanza Nchini Nigeria.    Vijana hao waliotoka katika mazingira magumu ikiwemo wengine kufiwa na Wazazi wao wameanza kidato Cha kwanza mwaka 2018 na Sasa wanarejea wakiwa wamehitimu kidato cha sita na baadae kurejea Tena Nchini Nigeria kwaajili ya kujiunga na chuo Kama anavyo tueleza meneja wa taasisi ya Tulia Trust Jacqueline Boaz. Wakiwa katika uwanja wa ndege wa Songwe Mkoani Mbeya vijana hao wamemshukuru Dkt Tulia Ackson Kwa kuwatoa sehemu ambayo walikua hawaelewi hatma ya elimu yao na Sasa wamefanikiwa kwa hatua kubwa kuhitimu kidato cha sita na kupata ufaulu Mzuri wa kwenda chuo kikuu Nchini Nigeria, huku baadhi ya walezi wakieleza maisha ya awa...

SHUJAA BULUGU ATOA SHUKRANI KWA KAMANDA WA POLISI (RPC) MKOA WA MWANZA KWA MWALIKO WAKE KWA SMAUJATA KUSHIRIKI SHEREHE YA UVISHWAJI NISHANI KWA MAAFISA , WAKAGUZI , NA ASKARI WA KANDA YA ZIWA

Image
Mwenyekiti SMAUJATA Taifa Shujaa Sospeter Mosewe Bulugu analipongeza na kulishukuru jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza kwa Mwaliko huo ambapo Mwenyekiti SMAUJATA Mkoa wa Mwanza Shujaa Gasto Alex Didas (Aliyevaa Suti nyeusi Mstari wa Pili) kwa niaba ya Mwenyekiti SMAUJATA Taifa amehudhuria na Kushiriki. Katika Sherehe hiyo, Mgeni Rasmi ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Afande IGP Camillius Mongoso Wambura ambapo amewavisha nishani Maafisa na Maaskari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kwa Niaba ya Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan . Jumuiya ya SMAUJATA Itaendelea Kufanya Kazi na Kushirikiana Bega kwa Bega (Sako kwa Bako) na Jeshi la Polisi Nchini katika Mapambano dhidi ya Vitendo vya ukatili na Katika Shughuli zote za Ustawi wa Jamii. Shujaa Sospeter Mosewe Bulugu ,  Mwenyekiti SMAUJATA Taifa By Wamzi Media

TK MOVEMENT YAZINDULIWA DODOMA MEI 25,2024, WAZIRI NDEJEMBI AWAAGIZA WATENDAJI KUTOA USHIRIKIANO KWA VIJANA

Image
Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Watendaji wa Kata, Mitaa, Vijiji, Taasisi na Asasi mbalimbali wameombwa kuwapa vijana ushirikiano wa kutosha wanapopita katika maeneo yao kukutana na vijana wenzao kubadilishana mawazo na kuwapa mafunzo ya namna ya kujikwamua kiuchumi kwa kutumia fursa. Agizo hilo limetolewa Mei 25 na Waziri wa Nchini, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Watu wenye Ulemavu na  Deogratias Ndejembi wakati akizindua Mtandao wa Kitaifa wa Vijana wa  Taifa Letu, Kesho yetu iliyobora (TK Movement), uzinduzi ambao umewakutanisha vijana kutoka mikoa yote nchini na kuhudhuriwa na viongozi na watendaji kadhaa wa Serikali na Bunge. Waziri Ndejembi amesema ushirikiano huo unalenga kuwapatia vijana waliopo pembezoni mwa mikoa furusa zilizopo katika maeneo yao pamoja na kuendelea kuyazungumzia mema na mazuri yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya sita. Amesema haoni  sababu ya kukataa ombi hilo la kupatiwa ushiri...

KUOGA KILA MARA SIO AFYA, OGA MARA MBILI KWA WIKI

Image
Daktari bingwa wa tiba ya uzuwiaji wa magonjwa James Hamblin alifanya utafiti kuhusu utakatishaji wa ngozi ambao hivi karibuni umechapishwa katika kitabu.  "Ninajihisi vizuri kabisa ,"alijibu dokta James Hamblin alipoulizwa anajihisi vipi baada ya kuishi bila kuoga kwa kipindi cha miaka mitano. " Unazowea tu", Hamblin ana umri wa miaka 37, na ni mtaalamu aliyesomea taaluma yake katika Chu kikuu cha Yale University kitengo cha huduma ya afya ya umma na ni daktari bingwa wa tiba ya kuzuia magonjwa.  CHANZO CHA PICHA,   GETTY IMAGES Maelezo ya picha,  Hamblin hatahivyo anasisitizia juu ya umuhimu wa kunawa mikono kwa sabuni lakini anasema sio lazima kuosha sehemu nyingine za mwili mara kwa mara Ni mmoja wa waandishi wa jarida la Marekani -The Atlantic , ambamo aliandika taarifa iliyokuwa na kichwa cha habari kinachosema :Niliacha kuoga , na maisha yangu yameendelea vyema.  "Tunatumia miaka muda wa miaka miwili maishani mwetu kwa kuoga tu. Muda huo unaweza kuzalish...

HISTORIA YA WANYAKYUSA

Image
         Historia inasema kwamba asili ya Wanyakyusa ni mkoani Morogoro. Kabila hilo likitokana na kabila la Waluguru. Hili hasa ndilo chimbuko la Wanyakyusa.         Inasemekana kwamba mwindaji mmoja wa Kiluguru alitembea peke yake porini bila ya kuongozana na mtu mwingine. Alitembea hadi akafika maeneo ya Kabale huko Suma, Tukuyu wilayani Rungwe. Akiwa huko, akaendelea na kazi yake ya uwindaji. Baadaye akatokea Mzulu mmoja kutoka Afrika Kusini aliyekuwa na binti yake. Akafika maeneo alikokuwa akiishi yule mwindaji Mluguru, naye akapiga kambi hapo Kabale, wakaungana katika maisha ya uwindaji.          Ikawa kila yule Mluguru akitoka asubuhi kwenda kuwinda, alikuwa akifanikiwa kurejea nyumbani na wanyama wakati rafiki yake wa Kizulu alikuwa akirudi mikono mitupu.        Kutokana na hali hiyo, Mluguru akageuka kuwa mfadhili wa Mzulu, kwa kutoa misaada mara kwa mara, na kwa kulipa fadhila hizo, akamw...